Monday, November 26, 2012
TIMU YA RWNANDA ILIYOKO KATIKA MASHINDANO LEO IMEWEZA KUIBUKA NA USHINDI WA MABAO2-0,MAGOLI ALIYEFUNGA NI MSHAMBULIAJI WA, WA TIMU YA YOUNG AFRICAN SPORT CLUB NIYONZIMA DAKIKA 79.

TIMU YA RWNANDA ILIYOKO KATIKA MASHINDANO LEO IMEWEZA KUIBUKA NA USHINDI WA MABAO2-0,MAGOLI ALIYEFUNGA NI MSHAMBULIAJI WA, WA TIMU YA YOUNG AFRICAN SPORT CLUB NIYONZIMA DAKIKA79
Sunday, November 25, 2012
![]() |
| JOHN BOCCO,NDIYE ALIYEFUNGA MAGOLI YOTE2-0. |
| MSUVA AKIMTOKA MCHEZAJI WA SUDAN. |
| MASHABIKI WA TANZANIA WAKIJA KUWAPA SUPPORT TIMU YAO. |
TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania Bara, imeanza vema kampeni zake za kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge, baada ya kuichapa mabao 2-0 Sudan katika mchezo uliomalizika usiku huu kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole, Kampala, Uganda.
Ushindi huo, unaiweza Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Kundi B, nyuma ya Burundi inayoongoza kwa wastani wa mabao.
Hadi mapumziko, Stars walikuwa mbele kwa mabao 2-0, yote yakipachikwa kimiani na mshambuliaji wa Azam FC, John Raphael Bocco ‘Adebayor’ aliyetumia vema krosi za Mrisho Khalfan Ngassa.
Bocco alifunga bao la kwanza Bocco aliiwahi vema krosi ya Ngassa aliyewatoka mabeki wa Sudan wingi ya kushoto na kuitumbukiza kimiani dakika ya 14.
Adebayor wa Chamazi aliwainua tena vitini mashabiki wa Tanzania dakika ya 28, akiunganisha krosi ya Ngassa tena kutoka kule kule kushoto.
Kwa ujumla Tanzania Bara walicheza vizuri kipindi cha kwanza, wakishambulia zaidi kupitia pembeni, kulia Simon Msuva ambaye hakuwa na madhara sana na kushoto Ngassa ambaye alikuwa mwiba mchungu haswa kwa Wasudan.
Pamoja na Bara kutawala kipindi cha kwanza, lakini Wasudan walifanya mashambulizi kadhaa ya kushitukiza na sifa zimuendee mlinda mlango Juma Kaseja, ambaye alioko amichomo miwili ya hatari mno.
Kipindi cha pili Stars, inayofundishwa na Mdenmark Kim Poulsen iliendelea kutawala mchezo, lakini safu ya ulinzi ya Sudan iligangamala.
Tanzania Bara; Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Amir Maftah, Shomari Kapombe, Kevin Yondan, Frank Domayo, Salum Abubakar/Amri Kiemba, John Bocco, Mwinyi Kazimoto na Simon Msuva/Shaaban Nditi.
Sudan; Ebd Elrahman Ali, Moawia El Amin, Sami Abdallah, Faris Abdallah, Hamoda Bashir/Farid Mohamed, Mohamed El Mortada, Sadam Abutalib, Mohamed Mussa Idris, Modathir Mohamed, Adam Sayer/Osama El Rashid na Mohamed Osman/Saed Siddig.
Katika mchezo wa awali, Burundi walishinda mabao 5-1, mabao yake yakifungwa na Chris Nduwarugira dakika ya 35 na 88, Yussuf Ndikumana dakika ya 41 na Suleiman Ndikumana dakika ya 84 na 90, wakati la Somalia lilifungwa na Mohamed Jabril kwa penalti dakika ya 55.
Matokeo hayo yanalifanya Kundi B lizidi kuwa gumu, kwani Burundi inaongoza kwa pointi zake tatu na mabao mengi, Tanzania ya pili kwa pointi tatu na mabao mawili- lakini bado Sudan wanaweza kupata matokeo mazuri katika mechi zijazo.
NENO LA LEO LANGU
MUNGU BARIKI TANZANIA MUNGU BARIKI WACHEZAJI WAKE.
Saturday, November 24, 2012
TIMU ya
taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars imelalamikia Uwanja mbovu wa Chuo
Kikuu cha Kampala Kampasi ya Biashara, waliopelekwa kufanya mazoezi leo
kujiandaa na mechi ya kesho ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati,
CECAFA Tusker Challenge 2012 dhidi ya Sudan, itakayopigwa kwenye Uwanja wa
Mandela, Namboole mjini hapa.
Ofisa Habari
wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniphace Wambura amewasilisha malalamiko
hayo kwa Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Uganda (FUFA), Rodgers Mulindwa
ambaye ameahidi kuyafanyia kazi.
“Tutalifanyia
kazi suala hilo, tutakuwa na kikao kesho litawasilishwa na litapatiwa usumbufu,
mwanzo huwa na matatizo, lakini mambo yatakuwa mazuri,”alisema
Mulindwa.
Hata hivyo,
inashangaza Stars kupelekwa katika Uwanja wa Chuo Kikuu cha Kampala Kampasi ya
Biashara, wakati kwenye mpango wa awali kabisa wa FUFA ilitakiwa kufanya mazoezi
kwenye Uwanja wa Nakawa.
Kwa upande
wake, kocha wa Kilimanjaro Stars, Mdenmark Kim Poulsen amesikitishwa na
kutowasili kwa washambuliaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe ya
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
“Mbwana
Samatta na Thomas Ulimwengu wanaweza wasicheze katika mechi ya kesho kwa sababu
hawajafika, lakini mimi nikiwa kocha nimejiandaa vizuri na nina imani na
wachezaji waliopo,” alisema.
“Nina imani
TFF wanafuatilia suala hili na wachezaji hawa watajiunga na wenzao hivi karibuni
lakini hii haituzuii kufanya vizuri kwani tumejiandaa vizuri,”
alisema.
Alisema
wachezaji wote wana hali nzuri na wana ari ya kushinda mechi yao ya kwanza dhidi
ya Sudan ambazi zimo katika Kundi B pamoja na Burundi na Somalia
Subscribe to:
Comments (Atom)























